Friday, February 26, 2016

BARCELONA YAFANIKIWA KUMTULIZA NEYMAR.

KLABU ya Barcelona imefanikiwa kuzipiku Real Madrid, Manchester United, Manchester City pamoja na Paris Saint-Germain kwa kumshawishi nyota wake Neymar kusaini mkataba mwingine mpya wa miaka mitano. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil ambaye alimaliza katika nafasi ya tatu kwenye tuzo za Ballon d’Or anadaiwa kusaini mkataba huo mpya ambao utamuweka Camp Nou mpaka mwaka 2021 na kumfanya kuwa mchezaji wa pili anayelipwa zaidi katika timu hiyo baada ya Lionel Messi. Mustakabali wa Neymar ulikuwa ukitiliwa shaka haswa kutokana na kesi ya masuala ya kodi inayomuandama hali ambayo ilizua tetesi kuwa anaweza kuondoka majira ya kiangazi. Hata hivyo, kumshawishi nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 kusaini mkataba mwingine ni hatua nzuri kwa klabu hiyo ambayo aliisaidia kushinda mataji matano mwaka uliopita pekee.

No comments:

Post a Comment