Friday, February 26, 2016

VAN GAAL AMPONGEZA MARCUS RASHFORD.

MENEJA wa Manchester United, Louis van Gaal amempongeza Marcus Rashford kwa ushujaa alioonyesha katika ushindi wa mabao 5-1 waliopata dhidi ya Midjylland katika mchezo wa Europa League uliofanyika jana. Katika mchezo huo Rashford alifunga mabao mawili ndani ya dakika ya 12 ukiwa ni mchezo wa kwanza kupangwa katika kikosi cha kwanza kufuatia kuumia kwa Anthony Martial dakika za mwishoni. Chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 18 sasa anakuwa ameipita rekodi iliyowekwa na George Best ya mchezaji mdogo zaidi katika klabu hiyo kufunga katika michuano ya Ulaya. Akihojiwa Van Gaal amesema kipindi cha kwanza Rashford alikuwa akikimbia sana maeneo ya pembezoni hivyo ilivyofika mapumziko alimrekebisha na kumwambia aingie ndani zaidi kwani anaweza kufunga na ndivyo ilivyotokea. United sasa wanakuwa wamesonga mbele kwa jumla ya mabao 6-3 baada ya kupoteza mchezo wa mkondo wa kwanza uliofanyika Denmark kwa mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment