Friday, February 26, 2016

RATIBA EUROPA LEAGUE: LIVERPOOL VS MAN UNITED.

KLABU ya Liverpool imepangwa kucheza na mahasimu wao Manchester United katika hatua ya timu 16 bora ya michuano ya Europa League. Kwa upande wa Tottenham Hotspurs wao wamepangwa kucheza na wakongwe wa soka wa Ujerumani Borussia Dortmund. Valencia wanaonolewa na Gary Neville wanatarajiwa kupambana na wapinzani wao katika La Liga Athletic Bilbao, wakati wa mabingwa watetezi wa michuano hiyo Sevilla wao watakuwa wageni wa FC Basel ya Uswisi ambao uwanja wao ndio uliotumika katika fainali iliyopita. Mechi hizo zinatarajiwa kuchezwa Alhamisi ya Machi 10 na 17 ambapo mshindi wa michuano wa michuano hiyo atafuzu moja kwa moja michuano ya Ligi ya Mabingwa msimu ujao.

Ratiba kamili ya michuano hiyo ni kama ifuatavyo.Shakhtar Donetsk v Anderlecht
Basel v Sevilla
Villarreal v Bayer Leverkusen
Athletic Bilbao v Valencia
Liverpool v Manchester United
Sparta Prague v Lazio
Borussia Dortmund v Tottenham
Fenerbahce v Braga

No comments:

Post a Comment