Friday, February 26, 2016

DFB KWAWAKA MOTO: BAADA YA RAIS SASA KATIBU MKUU.

KATIBU mkuu wa Shirikisho la Soka la Ujerumai-DFB, Helmut Sandrock amejiuzulu wadhifa wake huo akidai kashfa ya ufisadi iliyolikumba shirikisho hilo kuwa inahitaji watu wapya. Sandrock anakuwa ofisa wa pili wa ngazi ya juu ya DFB kujizulu kufuatia rais wa zamani Wolfsgang Niersbach kufanya hivyo kufuatia kashfa ya kulilipa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA ili waweze kuhakikisha wanapata uenyeji wa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2006. DFB inatarajia kuwasilisha taarifa yake kutoka tume huru kuhusiana na masuala hayo wiki ijayo huku pia ikitarajia kumpigia kura Reinhard Grindel kuwa rais wake mpya Aprili mwaka huu. Katika taarifa yake Sandrock amesema kwa mustakabali wa soka lao na DFB ni lazima kuanza upya ndio maana ameamua kujiuzulu ili kuwapisha viongozi wengine watakaochaguliwa.

No comments:

Post a Comment