Friday, February 26, 2016

UCHAGUZI FIFA: SASA UKOMO NI VIPINDI VITATU PEKEE, SEXWALE AJITOA DAKIKA ZA MAJERUHI.

RAIS atakayechaguliwa kuliongoza Shirikisho la Soka Duniani-FIFA anatarajiwa kuwa ukomo wa uongozi wa vipindi vitatu baada ya shirikisho hilo kuamua kupitisha mageuzi hayo ili kujinasua kutoka katika janga la ufisadi linaloikabili kwasasa. Baraza jipya linatarajia kuchukua nafasi ya kamati ya utendaji ya sasa huku kukiwapo na kila mwakilishi mwanamke kutoka katika kila shirikisho. Mageuzi hayo yalitangazwa leo katika mkutano mkuu maalumu uliofanyika jijini Zurich, ambayo pia yameamua kuweka wazi suala la mishahara. 
Wakati wowote kuanza sasa FIFA itapata rais mpya atakayechukua mikoba ya Sepp Blatter ambaye ameliongoza shirikisho hilo kwa miaka 18 yenye vipindi vitano. Wagombea wamebaki wanne wanaogombea nafasi hiyo ambao ni Sheikh Salman bin Ebrahim al-Khalifa wa Bahrain, Gianni Infantino ambaye ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA, Prince Ali bin al-Hussein wa Jordan na Jerome Champagne wa Ufaransa baad ya Tokyo Sexwale wa Afrika Kusini kujitoa dakika za mwisho.

No comments:

Post a Comment