Saturday, February 27, 2016

CHIELLINI FITI KUIVAA INTER.

KLABU ya Juventus imethibitisha beki wake Giorgio Chiellini yuko fiti na anaweza kurejea katika mchezo wa Serie A dhidi ya Inter Milan utakaochezwa baadae leo. Chiellini alikosa mechi tatu zilizopita za Juventus kutokana na kusumbuliwa na matatizo ya msuli aliyopata katika mchezo dhidi ya Frosinone ambao walishinda mabao 2-0. Hata hivyo, beki huyo mwenye umri wa miaka 31, ametajwa katika kikosi cha wachezaji 23 ambacho kitakuwa ugenini leo kuivaa Inter Milan. Meneja wa Juventus, Massimiliano Allegri pia amewajumuisha Kwadwo Asamoha na Alex Sandro katika kikosi hicho.

No comments:

Post a Comment