Sunday, February 28, 2016

KLOPP APANIA KUIHARIBIA CITY.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema ana hamu ya kutwaa Kombe la Ligi wakati kikosi chake kikijitupa uwanjani kukwaana na Manchester City katika mchezo wa fainali utakaofanyika katika Uwanja wa Wembley. Meneja huyo raia wa Ujerumani anategemea mchezo mgumu kutoka kwa City haswa kutokana na timu hiyo kurejea katika kiwango chao kwa ushindi mzuri waliopata katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Dynamo Kiev uliochezwa katikati ya wiki. Klopp ana matumaini ya kutwaa taji lake la kwanza akiwa Na Liverpool baada ya klupita miezi mitano pekee toka akabidhiwe mikoba ya kuinoa. Akihojiwa Klopp amesema anafahamu kuwa City wako vizuri kwasasa na utakuwa mchezo mgumu lakini ana hamu kubwa ya kushinda taji hilo.

No comments:

Post a Comment