Sunday, February 28, 2016

LAMPARD AHOFIA MUSTAKABALI WA CHELSEA PINDI TERRY ATAKAPOONDOKA.

KIUNGO wa zamani wa kimataifa wa Uingereza, Frank Lampard amesema ana mashaka kuhusu mustakabali wa Chelsea baada ya John Terry kuondoka katika klabu hioyo. Nahodha huyo anatarajiwa kuondoka Stamford Bridge majira ya kiangazi kufuatia kubainisha Januari kuwa mkataba wake wa sasa hautaongezwa. Lampard, ambaye aliondoka katika klabu hiyo mwaka 2014 baada ya kuitumikia kwa zaidi ya muongo mmoja, anadhani Chelsea wako hatarini kupoteza utambulisho wake. Kiungo huyo mkongwe amesema kinachomuogopesha ni kuhusu suala la haiba ya kweli katika timu pindi Terry atakapoondoka.

No comments:

Post a Comment