Wednesday, February 24, 2016

BARCELONA NDIO TIMU BORA DUNIANI - SUAREZ.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Luis Suarez amesisitiza kuwa malengo yao makubwa ni kutetea taji lao la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuifunga Arsenal kwa mabao 2-0 jana. Mabao mawili yaliyofungwa na Lionel Messi katika kipindi cha pili yalitosha kuwapa uongozi Barcelona katika mchezo huo wa mkondo wa kwanza hatua ya 16 bora uliofanyika katika Uwanja wa Emirates. Barcelona wanaonolewa na Luis Enrique wamepania kutetea taji lao hilo ili ije kuwa timu ya kwanza kuwahi kufanya hivyo toka AC Milan walivyofanikiwa miaka 25 iliyopita. Akihojiwa Suarez amesema wana matamanio makubwa ya kutaka kuendelea kushinda mataji kwasababu wana kikosi bora kabisa duniani.

No comments:

Post a Comment