Wednesday, February 24, 2016

MENSAH AENDA ANZHI.

BEKI wa kimataifa wa Ghana, Jonathan Mensah amesaini mkataba wa miaka miwili na nusu na klabu ya Anzhi Makhachkala ya Urusi. Beki huyo mwenye umri wa miaka 25, alikuwa akiichezea klabu ya ligi daraja la pili ya Ufaransa, Evian Thonon Gaillard ambapo mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu. Sasa Mensah anatarajiwa kujiunga na kikosi cha Anzhi wakati watakapokuwa katika kambi ya mazoezi ya majira ya baridi nchini Hispania. Mensah alishinda taji la Kombe la Dunia mwaka 2009 akiwa na kikosi cha timu ya taifa ya Ghana cha vijana chini ya umri wa miaka 20 na amewahi kukichezea kikosi cha wakubwa katika Kombe la Dunia mwaka 2010 na 2014.

No comments:

Post a Comment