Wednesday, February 24, 2016

INFANTINHO ANA UHAKIKA WA KUPATA KURA NYINGI AFRIKA.

MGOMBEA urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Gianni Infantino ana uhakika kuwa atakusanya kura nyingi kutoka mataifa ya Afrika katika uchaguzi Ijumaa hii. Infantino alifnya ziara fupi Afrika Kusini kwa mwaliko wa hasimu wake katika kinyang’anyiro hicho Tokyo Sexwale ambapo wawili hao walikutana katika kisiwa cha Robben, gerea ambalo Sexwale aliwahi kufungwa katika kipindi cha ubaguzi wa rangi. Kisiwa cha Robben pia ndio ambako rais wa zamani wa Afrika Kusini Hayati Nelson Mandela alifungwa. Lakini pamoja na Shirikisho la Soka la Afrika-CAF kutoa msimamo wake kuwa watamuunga mkono Sheikh Salman bin Ibrahim al-Khalifa wa Bahrain, katibu mkuu huyo wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA ameema ana uhakika wa kuungwa mkono na mataifa ya Afrika.

No comments:

Post a Comment