Monday, February 22, 2016

NILIKATAA OFA YA MAN UNITED - VIDAL.

KIUNGO wa Bayern Munich, Arturo Vidal amebainisha alikataa uhamisho wa kwenda Manchester United ili aweze kujiunga na mabingwa wa Bundesliga. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 aliondoka Juventus kuelekea Allianz Arena kiangazi mwaka jana lakini pia alikuwa amepata ofa kadhaa kutoka klabu zingine wakiwemo United. Vidal amesema kulikuwa na nafasi ya kwenda kujiunga na United lakini alibadili mawazo yake na kuamua kujiunga na Bayern. Mchezaji huyo aliendelea kudai kuwa alipenda nafasi ambayo United walimpatia lakini haikuwezekana na kuamua kwenda Ujerumani.

No comments:

Post a Comment