Thursday, February 25, 2016

RAIS WA ZAMANI WA BAYERN ATAKA KUBAKIA MSHABIKI WA KAWAIDA BAADA YA KUTOKA GEREZANI.

RAIS wa zamani wa Bayern Munich, Uli Hoeness amesema anataka kubakia kuwa mshabiki pekee kufuatia kuachiwa kutoka jela juzi ambako ametumikia nusu ya kifungo chake kutokana na makosa ya ukwepaji kodi. Hoeness ametumikia miezi 21 jela katika miaka mitatu ya kifungo chake baada ya kuhukumiwa Machi mwaka 2014 kufuatia kukutwa na hatia ya kukwepa kodi inayofikia euro milioni 28.5. Hoeness alitumikia kifungo chake katika gereza la Landsberg na alikuwa akitumikia kifungo cha nje toka Januari mwaka 2015 ambapo alikuwa akifanya kazi katika akademi ya vijana ya Bayern nyakati za mchana na kurejea jela jioni. Akihojiwa Hoeness amesema kwasasa anataka kufurahia soka na jambo kubwa atakalokuwa akifanya ni kwenda uwanjani na kushuhudia mechi kama mshabiki wa kawaida. Hoeness amewahi kuitumikia Bayern akiwa mchezaji, meneja na rais katika kipindi cha miongo minne iliyopita.

No comments:

Post a Comment