Sunday, February 21, 2016

ROBO FAINALI FA: CHELSEA KUIVAA EVERTON.

KLABU ya Chelsea itasafiri kuwafuata mahasimu wao wa Ligi Kuu Everton katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la FA. Chelsea jana walifanikiwa kuirarua Manchester City kwa mabao 5-1 katika mchezo wa mzunguko wa tano uliofanyika katika Uwanja wa Stamford Bridge. Manchester United na Shrewsbury inayoshiriki ligi daraja la kwanza wao watacheza mchezo wao baadae leo ambapo mshindi atakuwa mwenyeji wa West Ham United. Mechi za robo fainali ya FA itazikutanisha Reading dhidi ya Crystal Palace wakati Watford wanasubiri mshindi katika mchezo wa marudiano kati ya mabingwa watetezi Arsenal dhidi ya Hull City. Mechi za robo fainali zinatarajiwa kuchezwa mwishoni mwa wiki ya Machi 11 na 14 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment