Sunday, February 21, 2016

PICHA ZA PELE NA KIKOSI CHA BRAZIL KATIKA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA MWAKA 1966 NCHINI UINGEREZA.

PICHA za kipekee za Pele na kikosi cha Brazil kilichoshinda kombe la dunia la mwaka wa 1966 zimetolewa kwa mara ya kwanza. Picha hizo zinaonesha kikosi hicho kinachomjumuisha gwiji wa kandanda Pele wakibarizi nje ya mgahawa wa kifahari huko Cheshire Uingereza . 
Picha hizo ni sehemu ya onyesho moja katika mgahawa wa Lymm. Hoteli hiyo ya Lymm ndio iliyokuwa makao ya kikosi hicho wakati wa mchuano huo yapata miaka 50 iliyopita. Moja wa wachezaji nyota katika enzi hizo Pele na Garrincha wanaonekana wakijivinjari. Baadhi ya picha hizo zilipigwa na meneja wa magahawa huo Roger Allen. 
Meneja wa sasa wa hoteli hii ya Lymm, Jamie McDonald, anasema: "Babu yangu hakuisha kuzungumzia uwezo wa gwiji Pele. ''Alinieleza kuwa wakati huo wachezaji walikuwa wanyenyekevu mno ,hata wengine waliomba wenyeji baiskeli ilikupasha misuli moto'' Pele,wakati huo ndiye aliyekuwa ameuteka ulimwengu kwa miondoko yake na ilikumzuia asisumbuliwe na wapiga picha iliwabidi kukodishiwa hoteli ya kipekee yenye uwezo wa kuwalinda. 
Glenda Bowers, alikuwa na miaka 15 wakati huo. "mimi na mwenzangu tulikuwa wachanga kwa hivyo tuliruhusiwa kukutana na wachezaji hao'' Baadhi ya bidhaa zinazooneshwa ni pamoja na soksi na viatu zilizokuwa za Pele. "alimpatia mhudumu wa ndani aliyekuwa akifua nguo zao ikiwemo suruali fulana na hata sare moja.'' Pia kunapicha ambayo pele alipigwa pamoja na muhudumu wa baa bi Bessie Vale. 
Wakati huo Pele alikuwa ameapa kutocheza tena katika kombe la dunia akidai wachezaji weupe walimpiga mateke mengi mno katika uwanja wa Goodison Park. Uwanja huo wa Goodison Parkndio unaotumika na klabu inayoshiriki ligi kuu ya Uingereza ya Everton. Onyesho hilo lenye nembo ya ''BrazilLymm66'', litaendelea kwa siku nne.

No comments:

Post a Comment