Thursday, February 25, 2016

RONALDO ASISITIZA HANA MPANGO WA KUONDOKA MADRID.

MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amesisitiza kuwa na furaha katika klabu hiyo na hana mpango wowote wa kuondoka. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno amekuwa akihusishwa na tetesi za kuondoka Santiago Bernabeu katika siku za karibuni huku Paris Saint-Germain ikitajwa kama timu atakayokwenda. Lakini pamoja na kukosolewa kiwango chake msimu huu na tetesi zilizozagaa kuhusu mustakabali wake, Ronaldo amesisitiza bado anadhani anakubalika na mashabiki wa Madrid na anataka kuendelea kuwepo hapo kwa kipindi kirefu. Ronaldo amesema Madrid ni klabu yenye shinikizo kubwa ndani na nje ya uwanja lakini amekuwa hapo kwa miaka mingi hivyo ameshazoea.

No comments:

Post a Comment