Wednesday, February 24, 2016

SHABIKI WA LEICESTER ATAKA KUMPA BINTI YAKE JINA LA VARDY KAMA KUMBUKUMBU.

SHABIKI mmoja wa Leicester City ana matumaini ya kumpa jina la Jamie Vardy binti yake lakini kama ataungwa mkono vya kutosha ili kumshawishi mpenzi wake. Vardy ameng’ara ghafla katika soka la Uingereza msimu huu akivunja rekodi ya kushinda mechi 11 mfululizo za Ligi Kuu huku akiongoza kwa kutia nyavuni mabao 19 mpaka sasa. Sasa shabiki huyo Ashley Marriot anataka kuweka kumbukumbu ya msimu huu wa 2015-2016 ambao unaweza kumalizika kwa Leicester kuibuka mabingwa wa ligi, kwa kuongeza Vardy katika majina ya binti yake. Hata hivyo, suala hilo litakubaliwa na mpenzi wake Rebekah endapo tu ataungwa mkono za watu 5,000 katika mitandao.

No comments:

Post a Comment