Sunday, February 28, 2016

TETESI ZA USAJILI ZILIZOJIRI HUKO MAJUU.

KLABU ya West Ham United imemjumuisha Andre Ayew wa Swansea City katika orodha ya wachezaji wanaowahitaji majira ya kiangazi wakati wakijaribu kuimarisha safu ya ushambuliaji msimu ujao.
Chanzo: Daily Star

KLABU ya Real Madrid inadaiwa kumuwania mshambuliaji wa Sevilla Kevin Gameiro ambapo mahasimu wao wa La Liga wanatajwa kuwa hawatopokea chini ya euro milioni 40 kwa ajili ya nyota huyo.
Chnazo: Fichajes.net

SHIRIKISHO la Soka la Italia linamtaka meneja wa Leicester City Claudio Ranieri kuchukua nafasi ya Antonio Conte ambaye anatarajiwa kwenda Chelsea msimu ujao, baada ya kumalizika kwa michuano ya Euro 2016.
Chanzo: Fichajes.net

KLABU ya Manchester United inadaiwa kumfuatilia kwa karibu Andrew Robertson wa Hull City wakati huu wakiwa katika mawindo ya kutafuta beki wa kushoto. Chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 21 pia kiwnago chake kimewavutia Manchester City, Arsenal na Tottenham Hotspurs.
Chanzo: Daily Star

KLABU ya Chelsea inadaiwa kufikiria kumuwania beki wa Crystal Palace Scott Dann lakini wanaweza kulazimika kutoa kitita cha paundi milioni 20. Chelsea wamefikia hatua hiyo baada ya kuhofu John Stones anaweza kunyakuliwa na Manchestyer City.
Chanzo: Mail on Sunday

KLABU ya Arsenal inaendelea kumfuatilia kwa karibu kiungo wa Ajax Amsterdam Riechedly Bozoer. Maskauti wa Arsenal wanadaiwa kuwepo kwa karibu kila mchezo ambao chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 19 amekuwa akicheza.
Chanzo: The People


No comments:

Post a Comment