Monday, February 29, 2016

MESSI AFIKISHA MABAO 30 KWA MSIMU WA NANE MFULULIZO.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona Lionel Messi jana amefanikiwa kufikisha mabao 30 kwa msimu wa nane mfululizo wakati akiwasaidia mabingwa hao wa La Liga kutoka nyuma ya kuitandika Sevilla kwa mabao 2-1. Sevilla wanaoshika nafasi ya sita katika msimamo wa ligi ndio timu ya mwisho kuifunga Barcelona Octoba mwaka jana. Messi aliisawazishia Barcelona kwa bao la mipira wa adhabu baada ya Vitolo kuifungia Sevilla bao la kuongoza huku Gerard Pique akipigilia msumari wa mwisho. Barcelona ambao hawajafungwa katika mechi 34 zilizopita sasa wanaongoza ligi kwa tofauti ya alama nane huku wakiwazidi mahasimu wao Real Madrid kwa alama 12.

No comments:

Post a Comment