Monday, February 29, 2016

VAN GAAL RADHI KWA KUJIANGUSHA MBELE YA KAMISAA.

MENEJA wa Manchester United, Louis van Gaal ameomba radhi kwa kujiangusha mbele ya kamisaa wa mchezo wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ambao waliitandika Arsenal kwa mabao 3-2 jana. Meneja huyo raia wa Uholanzi alijiangusha mbele ya kamisaa huyo ili kujaribu kumwelewesha na kutoridhishwa kwake na maamuzi ya mwamuzi Mike Dean aliyechezesha pambano hilo. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Van Gaal amesema tukio alilofanya kalikuwa sahihi hivyo anaomba radhi kitendo hicho. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa alikuwa na hisia kubwa kwasababu ya aina ya mchezo wenyewe lakini anashukuru walipata matokeo waliyohitaji.

No comments:

Post a Comment