Monday, February 29, 2016

POCHETTINO APUUZA HABARI ZA UBINGWA.

MENEJA wa Tottenham Hotspurs, Mauricio Pochettino amesema wachezaji wake hawazungumzii suala la kushinda taji la Ligi Kuu msimu huu. Spurs wanashika nafasi ya pili katika msimamo wakiwa alama mbili nyuma ya vinara Leicester City baada ya kutoka nyuma na kuitandika Swansea kwa mabao 2-1 katika Uwanja wa White Hart Lane jana. Akihojiwa Pochettino amesema hakuna yeyote anayezungumzia ubingwa kwasasa katika vyumba vyao vya kubadilishia nguo. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa wanachoamini wao ni kushinda katika kila mchezo na kuona kitu gani kitatokea mwishoni mwa msimu. Wakiwa wamebaki ya mechi 11, Spurs wako alama tatu juu ya mahasimu wao Arsenal ambapo walifungwa na Manchester United jana. Hata hivyo Pochettino amesema kwa upande wake Arsenal kupoteza mchezo sio muhimu, na jambo muhimu kwake ni kuhakikisha wanacheza kwa kiwango chao bora kwani bado wana mechi nyingi zilizobaki.

No comments:

Post a Comment