Monday, February 29, 2016

CABALLERO ADAI PENATI ZA CITY ALIZOOKOA NI ZAWADI KWA PELLEGRINI KWA KUMUAMINI.

KIPA Manchester City, Willy Caballero amesema amemlipa meneja wake Manuel Pellegrini kwa kumuamini na kumpa nafasi ya kucheza katika fainali ya Kombe la Ligi iliyofanyika Wembley jana. Kipa huyo wa kimataifa wa Argentina aliokoa penati tatu za Liverpool na kuwafanya City kushinda kwa changamoto ya penati 3-1, baada ya timu hizo kutoka sare ya bao 1-1 katika muda wa kawaida. Caballero mwenye umri wa miaka 34, alikuwa akipondwa vikali baada ya kichapo cha mabao 5-1 walichopata katika mzunguko wa tano wa Kombe la FA kutoka kwa Chelsea wiki moja iliyopita. Akihojiwa Caballero ambaye alichukua nafasi ya kipa namba moja wa City, Joe Hart amesema alistahili kucheza katika fainali hiyo. Caballero ameanza katika mechi nne pekee za Ligi Kuu toka ajiunge na City akitokea Malaga Julai mwaka 2014.

No comments:

Post a Comment