Monday, February 29, 2016

RASHFORD APANIA KUENDELEZA MOTO ALIOANZA NAO.

MSHAMBULIAJI chipukizi wa Manchester United, Marcus Rashford anataka kuendelea moto wake alioanza nao katka kikosi cha kwanza cha United baada ya kuifungia timu yake mabao mawili muhimu katika mchezo dhidi ya Arsenal jana. Rashford mwenye umri wa miaka 18, alifunga mabao mawili wakati alipocheza kwa mara kwanza katika kikosi cha wakubwa kwenye ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Midtjylland ya Denmark katika mchezo wa Europa League Alhamisi iliyopita. Chipukizi huyo amerudia tena kufunga idadi hiyo ya mabao wakati alitambulishwa kwa mara ya kwanza katika Ligi Kuu na kuiwezesha United kuibuka ushindi muhimu wa mabao 3-1 dhidi ya Arsenal. Rashford amesema kujumuishwa kwake katika kikosi dakika za mwisho Alhamisi iliyopita baada ya Anthony Martial kuumia pengine ndio kulikomsaidia kufanya vyema. Nyota huyo amesema ni jambo zuri kuanza Ligi Kuu kwa kufunga na ana matumaini ya kuendelea kufanya hivyo ili kuisaidia timu yake.

No comments:

Post a Comment