Monday, February 29, 2016

WENGER AWATAKA WACHEZAJI WAKE KUSAHAU KIPIGO CHA UNITED NA KUZINGATIA MCHEZO WAO UJAO DHIDI YA SWANSEA.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amekitaka kikosi chake kusahau kipigo walichopata kutoka Manchester United na kujaribu kurejesha nguvu zao katika mbio za ubingwa katika mchezo dhidi ya Swansea City Jumatano hii. Pamoja na kipigo cha jana cha mabao 3-2 walichoapata Old Trafford, Arsenal wameendelea kushikilia nafasi ya tatu katika msimamo wa Ligi Kuu wakiwa alama tano nyuma ya vinara Leicester City. Akihojiwa kuelekea katika mchezo huo wa kesho kutwa Wenger amesema hawapaswi kujionea huruma kwani pamoja na kupoteza alama tatu muhimu lakini waliwaonyesha kuwa wanaweza kupambana. Kocha huyo ameendelea kudai kuwa wataendelea kupambana ili kuhakikisha wanapata matokeo mazuri katika michezo yao ijayo.

No comments:

Post a Comment