Monday, February 29, 2016

EL-CLASICO KUCHEZWA APRILI 2.

TAREHE rasmi ya mchezo wa marudiano ya Clasico ambayo huwakutanisha mahasimu wa Ligi Kuu ya Hispania Barcelona na Real Madrid imetangazwa. Timu hizo mbili zinatarajiwa kukwaana na Aprili 2 mwaka huu katika Uwanja wa Camp Nou ambapo Madrid watakwenda huko kujaribu kulipiza kisasi cha kutandikwa mabao 4-0 Novemba mwaka jana. Katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa Santiago Bernabeu, Barcelona ilipata mabao yake kupitia kwa nyota wake Luis Suarez aliyefunga mawili na moja kwa Neymar na Andres Iniesta huku Isco akionyeshwa kadi nyekundu dakika za majeruhi. Toka wakati huo Madrid waliamua kumtimua Rafa Benitez na nafasi yake kuchukuliwa na Zinedine Zidane lakini bado wamekuwa wakisuasua na kujikuta wakiachwa mbali na Barcelona katika msimamo wa La Liga.

No comments:

Post a Comment