Monday, February 29, 2016

TETESI ZA USAJILI ZILIZOJIRI HUKO MAJUU.

KLABU ya Real Madrid inadaiwa kuwahi kufikiria kumuwania kocha Mauricio Pochettino majira ya kiangazi lakini ilirudhishwa nyuma kwa sababu mbili kubwa ambazo ni uwezo wake kwa nyota atakaokuwa nao pamoja na rais wa Madrid kutotaka kufanya biashara tena na Daniel Levy.
Chanzo: El Pais

KLABU ya Real Madrid ilijaribu kumrejesha Jose Mourinho Santiago bernabeu baada ya Rafa Benitez kutimuliwa lakini wanadhani hatua yao hiyo ilitumiwa na kocha huyo pamoja na wakala wake Jorge Mendes kusaini mkataba wa awali wa makubaliano na Manchester United.
Chanzo: El Pais

KLABU ya Arsenal iko tayari kuingia katika vita vya kumuwania winga wa Leicester City Riyad Mahrez huku Manchester United, Chelsea, Barcelona na Real Madrid nazo zikihusishwa na tetesi za kumtaka nyota huyo wa kimataifa wa Algeria.
Chanzo: ESPN

KLABU ya Inter inajipanga kumpa ofa ya mkataba wa miaka mitano meneja wa Atletico Madrid Diego Simeone wenye thamani ya euro milioni 100, ili aweze kuwarejesha katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Chanzo: Fichajes.net

MENEJA wa AS Roma, Luciano Spalletti yuko tayari kumruhusu kiungo Daniele De Rossi kuondoka katika klabu hiyo msimu huu huku Los Angeles Galaxy wakiwa tayari kumpatia mkataba.
Chanzo: transfermarketweb.com

KLABU ya Deportivo La Coruna wamepanga kumrejesha La Liga kiungo wa Aston Villa Carlos Sanchez, majira ya kiangazi.
Chanzo: Gol Digital

No comments:

Post a Comment