Thursday, March 24, 2016

FA YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA WAHANGA WA BRUSSELS.

CHAMA cha Soka nchini Uingereza-FA kimetuma salamu zake za rambirambi kufuatia mashabulio ya mabomu huko Brussels kwa kuweka taa kuzunguka mnara wa Uwanja wa Wembley ambazo zina rangi ya bendera ya taifa ya Ubelgiji. Jumanne mashabulio kadhaa mabomu katika Uwanja wa Ndege na Stesheni ya Treni katika mji huo mkuu yalisababisha vifo vya watu 31 na wengine zaidi ya 270 kujeruhiwa. Nchi hiyo iko katika siku tatu za maombolezo kufuatia mashabulio hayo ya kigaidi. Mbali na uwanja wa Wembley lakini pia majengo mengine kadhaa yanayojulikana nchini Uingereza usiku yalikuwa yakiwaka taa za bendera la taifa hilo.

No comments:

Post a Comment