Tuesday, March 22, 2016

TETESI MBALIMBALI ZILIZOJIRI HUKO MAJUU.

MENEJA ajaye wa Manchester City, Pep Guardiola anataka kumuwania winga wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain kufuatia kumtaja katika orodha ya wachezaji wanne anaowahitaji.
Chanzo: Times

KLABU ya Real Madrid inadaiwa kuwepo katika mzungumzo na wakala Mino Raiola juu ya uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Everton Romelu Lukaku kwa kitita cha paundi milioni 60.
Chanzo: The Sun

MENEJA wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho anadaiwa kumtaka mkurugenzi wa michezo wa Atletico Madrid Andrea Berta kujiunga naye Old Trafford kama akiteuliwa kuchukua nafasi ya Louis van Gaal Manchester United.
Chanzo: Telegraph

KLABU ya Southampton inadaiwa kumfuatilia kwa karibu beki wa kushoto wa Walsall Rico henry ambaye anafananishwa na beki wa zamani wa kimataifa wa Uingereza Ashley Cole. Henry pia anadaiwa kuwaniwa na Liverpool, Arsenal, Leicester City na Swansea City.
Chanzo: Daily Mail

KLABU ya Tottenham Hotspurs inadaiwa kujipanga kumpa ofa ya mkataba mwingine Harry Kane ili kuzifukuza klabu ambazo zinataka kumuwania.
Chanzo: Football Insider

No comments:

Post a Comment