Tuesday, March 22, 2016

MSHAMBULIAJI WA NORWICH ANUSURIKA KATIKA MILIPUKO HUKO BRUSSELS.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Norwich City Dieumerci Mbokani ameponea chupuchupu katika milipuko iliyotokea katika Uwanja wa wa Ndege wa jijini Brussels leo. Mbokani mwenye umri wa miaka 30 alikuwa uwanjani hapo wakati milipuko miwili ilipotokea lakini klabu yake imesema mchezaji huyo sasa amesharejea nyumbani. Watu kadhaa wameuawa katika milipuko hiyo ambapo vyombo vya habari vimedai idadi yao imefikia 13. Waziri Mkuu wa nchi hiyo amesema matukio hayo yaliyotokea katika Uwanja wa Ndege na stesheni ya treni ni kigaidi.

No comments:

Post a Comment