Tuesday, March 22, 2016

QATAR KUTOA MALAZI KWENYE MAHEMA YA ASILI KOMBE LA DUNIA 2022.

MASHABIKI watakaokwenda kushuhudia michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022 litakalofanyika nchini Qatar wanaweza kupewa malazi katika mahema ya asili ya jangwani. Baadhi ya mashabiki kati ya 500,000 wanaotegemewa kwenda nchini humo wanaweza kupewa malazi katika mahema hayo ambayo yatakuwa karibu na viwanja. Msemaji wa kamati ya maandalizi ya michuano hiyo amesema watafanya hivyo ili kuonyesha ukarimu na urafiki wa watu wa Mashariki ya Kati.M Mahema hayo ya asili yanayojulikana kama Bedouin yatawawezesha mashabiki kulala huku wakiona nyota kwa juu. Michuano hiyo tayari imeshahamishwa kutoka muda wake uliozoeleka kwa Juni na Julai na kupelekwa Desemba kutokana na wasiwasi wa joto kali majira ya kiangazi.

No comments:

Post a Comment