Tuesday, March 22, 2016

PELLEGRINI ANATAKA KWENDA KUMNG'OA GARY NEVILLE.

MENEJA wa Manchester City, Manuel Pellegrini anadaiwa kutaka kuchukua mikoba ya kuinoa Valencia kutoka kwa Gary Neville katika kipindi cha majira ya kiangazi. Meneja huyo raia wa Chile anatarajiwa kuondoka City mwishoni mwa msimu huu huku meneja wa Bayern Munich Pep Guardiola akitarajiwa kuchukua nafasi yake. Vyombo vya habari nchini Chile vimekuwa vikidai kuwa Pellegrini mwenye umri wa miaka 62 anaweza kwenda Arsenal au Zenit St. Petersburg. Hata hivyo inadaiwa kuwa mwenyewe angependa zaidi kwenda Valencia kutokana na uzoefu alionao na La Liga kufuatia kuinoa Villarreal kwa miaka mitano kabla ya kwenda City.

No comments:

Post a Comment