Tuesday, March 22, 2016

DESCHAMPS AWATAKA WACHEZAJI WAKE KUSAHAU TUKIO LA PARIS.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps amesema kikosi chake kinapaswa kuendelea mbele wakati wakijiandaa kurejea tena Stade de France. Uwanja huo ulikuwa moja kati ya sehemu zilizolengwa katika mashambulio kadhaa yaliyotokea jijini Paris Novemba mwaka jana na kuua watu 130. Ufaransa ambao walikuwa wakicheza na Ujerumani wakati wa mashambulio hayo yakitokea, watarudi tena kwenye uwanja huo kuchuana na Urusi Machi 29 mwaka katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa. Akihojiwa Deschamps ambaye alikuwa kiungo wa zamani wa Chelsea, amesema hakuna anaweza kusahau yaliyotokea lakini hakuna haja ya kuzungumzia suala hilo kwani wanapaswa kuendelea mbele. Vikosi vya Ufaransa na Ujerumani wote walilazimika kulala uwanjani hapo baada ya tukio hilo la Novemba 13 huku milio ya milipuko ikisikika nje ya uwanja wakati wa mchezo.

No comments:

Post a Comment