Tuesday, March 22, 2016

CECH KIPA BORA CZECH.

KIPA wa kimataifa ya Jamuhuri ya Czech, Petr Cech ametangazwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa nchi hiyo. Cech Mwenye umri wa miaka 33, alichaguliwa na makocha, wachezaji na viongozi wa timu kutwaa tuzo hiyo kwa mara ya nane. Cech aliwazidi wachezaji wengine wa nchi hiyo waliokuwepo katika kinyang’anyiro hicho akiwemo mshambuliaji wa Sparta Praque David Lafata na kiungo wa Hertha Berlin Vladimir Darida. Cech anayekipiga Arsenal ameichezea nchi yake mechi 118 toka alipoitwa kwa mara ya kwanza mwaka 2002.

No comments:

Post a Comment