Tuesday, March 22, 2016

KIKOSI CHA UBELGIJI CHASITISHA MAZOEZI KUTOKANA NA MILIPUKO.

KIKOSI cha timu ya taifa ya Ubelgiji leo kimesitisha mazoezi yake kwa ajili ya heshima kwa wahanga wa shambulio lililofanyika jijini Brussels. Kikosi cha nchi hiyo kinatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Ureno katika Uwanja wa King Baudouin uliopo Brussels Machi 29 mwaka huu lakini sasa ratiba hiyo iko katika hatihati. Milipuko kadhaa ilitokea katika Uwanja wa Ndege wa mji huo pamoja na stesheni ya treni na kupelekea vifo vya watu 13. Ubelgiji imefuzu michuano ya Euro 2016 itakayofanyika Ufaransa na wamepangwa kundi E sambamba na timu za Italia, Jamhuri ya Ireland na Sweden.

No comments:

Post a Comment