Thursday, March 31, 2016

POGBA KUBAKIA JUVENTUS AKIKOSA DAU KUBWA.

WAKALA wa Paul Pogba, Mino Raiola amebainisha kuwa mteja wake huyo yuko tayari kusaini mkataba mpya na Juventus kama hakutakuwa na ofa kubwa mwishoni mwa msimu huu. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa, mkataba wake wa sasa unamalizika Juni 2019 lakini klabu kama Paris Saint-Germain, Barcelona, Manchester City na Chelsea zinadaiwa kumfuatilia kwa karibu. Pogba mwenye umri wa miaka 23, hana haraka ya kuondoka kwa mabingwa hao wa Serie A na anaweza kusaini mkataba mpya kama hatakubaliana na masharti ya mahali pengine. Akihojiwa Raiola amesema hakuna lililobadilika kwa Pogba kulinganisha na mwaka mmoja uliopita kwani kila kitu kikosi. Wakala huyo aliendelea kudai kuwa kama hakuna ofa nzuri itakayopatikana Pogba atafurahia kuendelea kubakia Juventus na wako tayari kufanya mazungumzo na mkataba mpya.

No comments:

Post a Comment