Thursday, March 31, 2016

FERGUSON ADAI LEICESTER WANASTAHILI KUWA MABINGWA LIGI KUU.

MENEJA wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson anaamini Leicester City wanastahili kutawadhwa mabingwa wa Ligi Kuu msimu huu. Leicester wamekuwa na msimu mzuri 2015-2016 wakiwa wanaongoza ligi kwa tofauti ya alama tano huku wakiwa wamebaki na mechi saba. Msimu uliopita wote ulikuwa wa wasiwasi kwa Leicester kwani walikuwa wakipigania kutoshuka daraja lakini hali imekuwa tofauti kwa mwaka huu. Hata hivyo, kutokana na ari na moyo wa kujituma walioonyesha chini ya Claudio Ranieri msimu huu, Ferguson anadhani hakuna timu inayostahili kushinda taji la ligi zaidi ya Leicester. Akihojiwa Ferguson ambaye alinyakuwa mataji 13 ya ligi akiwa na United amesema kwa uwezo mkubwa walioonyesha Leicester hana shaka kuwa wanastahili kushinda taji hilo.

No comments:

Post a Comment