Thursday, March 31, 2016

BILBAO YATHIBITISHA KUWA LAPORTE HATAWEZA KUMALIZA MSIMU.

KLABU ya Athletic Bilbao imethibitisha kuwa beki wake Aymeric Laporte ataukosa msimu wote uliobakia kwasababu ya kufanyiwa upasuaji kufuatia mguu wake uliovunjika wakati akiwa katika majukumu ya kimataifa. Beki huyo mwenye umri wa miaka 21 aliumia mguu wake wa kulia kufuatia kukwatuliwa wakati akikitumikia kikosi cha Ufaransa cha vijana chini ya umri wa miaka 21 dhidi ya Scotland Machi 24 mwaka huu. Bilbao imebainisha kuwa Laporte alifanyiwa upasuaji Jumanne na anatarajiwa kukaa nje kwa miezi minne hivyo kumfanya kukosa mechi zilizosalia msimu huu. Laporte amekuwa akihusishwa na tetesi na kuwania na Manchester City majira ya kiangazi huku taarifa zikidai kuwa meneja ajaye Pep Guardiola ameuweka katika orodha ya wachezaji anaowahitaji.

No comments:

Post a Comment