Thursday, March 31, 2016

PIGO BARCELONA, KUMKOSA MATHIEU CLASICO.

BEKI wa kimataifa wa Ufaransa na klabu ya Barcelona, Jeremy Mathieu anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa goti kutokana na majeruhi aliyopata wakati akiitumikia nchi yake Jumanne iliyopita. Taarifa ya klabu yake imedai kuwa kufuatia vipimo alivyofanyiwa imebainika kuwa Mathieu anatakiwa kufanyiwa upasuaji huo ili kurekebisha tatizo linalomkabili. Taarifa hiyo iliendelea kudai kuwa beki huyo anatarajiwa kufanyiwa upasuaji leo na madaktari wa klabu hiyo Ramon Cugat na Ricard Pruna. Mathieu mwenye umri wa miaka 32 alitolewa wakati wa mapumziko katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki ambao Ufaransa ilishinda mabao 4-2 dhidi ya Urusi huko Stade de France. Sasa beki huyo anatarajiwa kuukosa mchezo wa Clasico dhidi ya Madrid mwishoni mwa wiki hii huku kukiwa na wasiwasi pia wa kutokucheza kabisa msimu huu.

No comments:

Post a Comment