Thursday, March 31, 2016

RAMOS ATAMBA WATALIPA KISASI KWA BARCELONA.

BEKI wa Real Madrid, Sergio Ramos ana uhakika kikosi chao kinaweza kulipa kisasi dhidi ya mahasimu wao Barcelona wakati watakapokutana Jumamosi hii. Madrid walitandikwa mabao 4-0 katika mchezo wao wa kwanza uliofanyika katika Uwanja wa Bernabeu ambapo Luis Suarez alifunga mabao mawili na Neymar na Andres Uniesta wakifunga moja kila mmoja. Madrid walio chini ya Zinedine Zidane wamekuwa na msimu mgumu katika kampeni zao za La Liga ambapo kwasasa wako nyuma ya Barcelona kwa alama 10. Ramos pamoja na kikosi kizima cha Barcelona hawajashinda mchezo wa ligi nyumbani kwa Barcelona Camp Nou kw karibu miaka minne lakini nyota huyo wa kimataifa wa Hispania ana uhakika wanaweza kujirudi na kushinda mchezo huo.

No comments:

Post a Comment