Thursday, March 31, 2016

HODGSON AHAHA KUTAFUTA BEKI WA KATI, ATETA NA TERRY.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson amezungumza na John Terry wakati akiendelea kutafuta beki wa kati anayetumia mguu kushoto katik kikosi chake kuelekea michuano ya Euro 2016. Kikosi cha Uingereza kimefunga mabao manne katika mechi mbili za kimataifa za kirafiki zilizopita ambapo walishinda mabao 3-2 ugenini dhidi ya Ujerumani kabla ya kuchapwa mabao 2-1 nyumbani na Uholanzi. Gary Cahill na Chris Smalling ndio walioanza katika safu ya ulinzi katika mchezo wa Berlin kabla ya baadae kuungana na John Stones katika mchezo wa Wembley. Lakini beki wa kati imekuwa nafasi ambayo bado inalegalega katika kikosi cha Hodgson kuelekea michuano hiyo ya Ulaya mabapo Uingereza imepangwa sambamba na Urusi Wales na Slovakia katika kundi B.

No comments:

Post a Comment