Wednesday, March 30, 2016

MADRID WAJIPANGA KUFANYA KUFURU KWA AUBAMEYANG.

KLABU ya Real Madrid inadaiwa kujipanga kutoa ofa ya euro milioni 70 pamoja na Alvaro Morata ili waweze kumnasa mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang. Jarida la AS limedai kuwa Madrid bado wana nafasi ya kumsajili tena Morata kutoka Juventus kwa euro milioni 30, lakini wanatarajia kumtumia nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 ili waweze kumpata Aubameyang. Nyota huyo wa kimataifa wa Gabon amekuwa katika kiwango cha juu msimu huu akifunga mabao 35 katika mechi 40 za mashindano alizoichezea Dortmund msimu huu. Mapema wiki hii, Aubameyang ambaye pia amehusishwa na tetesi za kuwindwa na Arsenal, alikiri kuwa anaweza kukubali kujiunga na Madrid kama wakimuhitaji lakini alidai kwasasa bado ana mkataba na Dortmund unaomalizika 2020.

No comments:

Post a Comment