Wednesday, March 30, 2016

TEVEZ AKIRI KUKARIBIA KUJIUNGA NA ATLETICO KABLA YA KWENDA BOCA.

MSHAMBULIAJI wa Boca Juniors, Carlos Tevez amekiri alikaribia kujiunga na Atletico Madrid wakati alipoondoka Juventus mwishoni mwa msimu uliopita, lakini aliamua kurejea nyumbani. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina, alicheza misimu miwili Juventus na kushinda mataji mawili ya Serie A na kuisaidia kufika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Tevez alikuwa ameshaweka nia ya kurejea Argentina lakini amesema alipitiwa na wazo la kutaka kucheza Atletico chini Muargentina mwenzake Diego Simeone. Akihojiwa Tevez amesema Simeone alimpigia simu na alifurahia mawazo yake lakini hakuweza kuikatalia Boca Juniors.

No comments:

Post a Comment