Wednesday, March 30, 2016

HODGSON ADAI WACHEZAJI WAKE WALIKOSA UBUNIFU.

MENEJA wa timu ya taifa ya Uingereza, Roy Hodgson amesema amesikitishwa kutokana na kikosi chake kukosa ubunifu kufuatia kichapo cha mabao 2-1 walichopata kutoka kwa Uholanzi katika Wembley jana. Kipigo hicho kimekuja siku baada ya Uingereza kuionyesha kiwango bora wakitoka nyuma na kuwafuunga mabingwa wa dunia Ujerumani mabao 3-2. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Hodgson amesema pamoja na kumiliki vyema mpira lakini wachezaji wake hawakuwa wabunifu jambo lilichangia kutotengeneza nafasi za kutosha. Meneja huyo aliongeza kuwa hawakucheza vyema sana kama ilivyokuwa katika mchezo dhidi ya Ujerumani kule Berlin. Hicho kinakuwa kipigo cha kwanza kwa Uingereza katika Uwanja wa Wembley toka Novemba mwaka 2013.

No comments:

Post a Comment