Wednesday, March 30, 2016

MESSI AIBEBA ARGENTINA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Lionel Messi amefunga bao lake la 50 la kimataifa wakati akiisaidia Argentina kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Bolivia katika mchezo wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2018. Ushindi unaifanya Argentina kukwea mpaka nafasi ya tatu katika kundi lao wakiwa na alama 11 kutokana na mechi sita, alama mbili nyuma ya vinara Ecuador na Uruguay. Ecuador wao walipoteza mchezo wao wa kwanza katika kundi hilo wakifungw amabao 3-1 na Colombia wakati Uruguay walishinda bao 1-0 nyumbani dhidi ya Peru. Beki wa Argentina, Gabriel Mercado ambaye alifunga bao la ushindi katika mchezo wa Alhamisi iliyopita dhidi ya Chile ndio aliyefunga bao kuongoza dakika ya 21 katika mchezo huo kabla ya Messi hajafunga lingine kwa penati. Paraguay na Brazil wote wana alama tisa baada ya kutoka sare ya kufunga mabao 2-2 huko Asuncion jana. Timu nne za juu kati ya 10 zilizopo katika kundi hilo la nchi za Amerika Kusini ndio zitafuzu moja kwa moja fainali hizo za Kombe la Dunia wakati ile ya tano itakwenda katika hatua ya mtoano.

No comments:

Post a Comment