Wednesday, March 30, 2016

MOROCCO WAMEKUWA WA KWANZA KUFUZU AFCON.

MOROCCO imekuwa nchi ya kwanza kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika itakayofanyika mwakani nchini Gabon baada ya kuichapa Cape Verde mabao 2-0 huko Marrakech jana. Mshambuliaji nyota wan chi hiyo Youssef Al Arabi alifunga mabao hayo mawili mapema katika kipindi cha pili, bao moja likitokana na penati ambayo ilipelekea mchezaji wa Cape Verde kupewa kadi nyekundu. Morocco wamefikisha alama sita katika kundi F wakiongoza huku kukiwa kumebaki na mechi mbili hatua hiyo kukamilika. Mfaransa Herve Renard ambaye aliiongoza Zambia na Ivory Coast kunyakuwa taji la michuano hiyo katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita ndio aliyechukua mikoba ya kuinoa Morocco kutoka kwa Badou Zaki. Misri na Senegal nazo zinakaribia kufuzu michuano hiyo inayoshirikisha nchi 16 wakati Nigeria hali yao imekuwa mbaya pamoja na Afrika Kusini. Ushindi wa bao 1-0 waliopata Misri huko Alexandria umewafanya kujiimarisha kileleni mwa kundi G wakati Senegal nao walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Niger katika mchezo wa kundi K.

No comments:

Post a Comment