Wednesday, March 30, 2016

PELE AWASHITAKI SAMSUNG.

NGULI wa soka wa Brazil, Pele ameishitaki kampuni ya vifaa vya elektroniki ya Samsung akiidai fidia ya dola milioni 30 akiituhumu kampuni hiyo kutumia picha yake katika matangazo bila ruhusa yake. Kwa mujibu wa malalamiko yaliyopelekwa katika mahakama ya rufaa jijini Chicago, Samsung wanatuhumiwa kutumia picha inayofanana na nguli huyo katika tangazo lake huku kukiwa hakuna makubaliano yeyote baina yao. Pele mwenye umri wa miaka 75 ambaye jina lake kamili ni Edson Arantes do Nascimento, anahesabiwa kama mmoja wa wachezaji bora kabisa kuwahi kutokea duniani. Pamoja na kwamba tangazo hilo halimtaji Pele moja kwa moja lakini picha iliyotumika inadaiw kufanana kwa kila kitu na nguli huyo.

No comments:

Post a Comment