Wednesday, March 30, 2016

VILLA MAJANGA, GARDE AONDOKA.

MENEJA wa Aston Villa Remi Garde amejizulu wadhifa wake kwa maelewano baada ya kuinoa klabu hiyo kwa siku 147. Meneja huyo raia wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 49 alichukua mikoba ya Tim Sherwood akisaini mkataba wa miaka mitatu na nusu na klabu hiyo Novemba mwaka jana, lakini ameondoka baada ya kupokea vipigo sita mfululizo. Mechi ya mwisho kusimamia ilikuwa ile waliyochapwa bao 1-0 na Swansea Machi 19 mwaka huu, matokeo ambayo yameiacha Villa wakiburuza mkia huku wakidaiwa alama 12 ili waweze kujinasua kutoka nafasi hiyo. Villa wameshinda mechi mbili pekee kati ya 20 za ligi walizocheza chini ya Garde.

No comments:

Post a Comment