Wednesday, March 30, 2016

YAYA TOURE KUONDOKA MAN CITY.

WAKALA wa Yaya Toure, Dimitri Seluk amedai kuwa kiungo huyo anajiandaa kuondoka Manchester City na tayari wameshaanza mazungumzo na vilabu kadhaa Ulaya. Seluk aliwaonya City kuwa Toure ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu ujao, anaweza kuondoka labda wampe ofa ya mkataba mwingine kabla ya kumalizika kwa msimu. Lakini hakuna ofa yeyote aliyopewa nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast jambo ambalo limemfanya kuanza kutafuta mahali pengine huku klabu za Paris Saint-Germain, Bayern Munich na Juventus zikitajwa kumuwania. Seluk amesema tayari wameshaanza kuzungumza na vilabu vingine ili kujua wapi Toure ataelekea baada ya msimu kumalizika.

No comments:

Post a Comment