Thursday, March 24, 2016

UJERUMANI YATHIBITSIHA MECHI ZAKE KUENDELEA KAMA ZILIVYOPANGWA.

MKUU wa usalama wa Chama cha Soka cha Ujerumani-DFB amesema jana kuwa mechi za kirafiki za kimataifa zinazotarajiwa kuchezwa nyumbani kati ya Ujerumani dhidi ya Uingereza na Italia haziko katika hatari yeyote kufuatia mashabulio ya kigaidi jijini Brussels. Ofisa huyo, Hendrick Grosse-Lefert amesema hakuna ushahidi wowote unaonyesha kuwa kutakuwa na hatari katika mechi hizo zijazo. Hata hivyo, Lefert aliendelea kudai kuwa wanachukua tahadhari zote ili kuhakikisha michezo hiyo inachezwa katika hali ya usalama. Magaidi wa kujitoa mhanga walifanya mashabulio katika Uwanja wa Ndege jijini Brussels na stesheni ya treni na kusababisha vifo vya watu 31 na wengine 270 wakiachwa majeruhi. Ujerumani inatarajiwa kukwaana na Uingereza Jumamosi hii mbele ya mashabiki wapatao 72,000 wanaotarajiwa kutokea katika Uwanja wa Olimpiki uliopo jijini Berlin.

No comments:

Post a Comment