Thursday, March 24, 2016

DEL BOSQUE ADOKEZA KUENDELEA KUINOA HISPANIA.

KOCHA wa timu ya taifa ya Hispania, Vicente del Bosque amedokeza kuwa anaweza kuendelea kuinoa timu hiyo baada ya michuano ya Euro 2016. Del Bosque amekuwa kocha wan chi hiyo toka mwaka 2008 na kuwoangoza kushinda taji lao la kwanza la Kombe la Dunia mwaka 2010 na taji la pili mfululizo la michuano ya Euro 2012. Mkataba wa Del Bosque unatarajiwa kumalizika Julai 31, baada ya kumalizika michuano ya Euro itakayofanyika Ufaransa. Hata hivyo pamoja na siku za nyuma kudai michuano hiyo itakuwa ya mwisho, Del Bosque sasa ameonyesha kubadili mawazo na kudai anawez kuongeza siku.

No comments:

Post a Comment